RAIS WA FIFA AAHIDI NEEMA TANZANIA

Na Saida Salum. Dar es Salaam

Rais wa Shirikisho la mpira wa miguu duniani, (FIFA)  Gianny Infatinho amemuahidi Waziri mkuu wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania, Mhe Kassim Majaliwa kuwa Shirikisho lake litawekeza nchini.

Bosi huyo wa Fifa ameyasema hayo leo Magogoni Dar es Salaam alipomtembelea waziri mkuu, Infantinho amedai Tanzania ni sehemu nzuri kuwekeza kutokana na amani na utulivu uliopo.

Uongozi wote wa Shirikisho la soka ulimwenguni pamoja na wa mabara yote waliwasili jana nchini kuanza mkutano mkubwa wa Shirikisho hilo ambapo Tanzania inawakilishwa na Rais wa Tff, Wallace Karia, Kaimu katibu mkuu, Wilfred Kidao na mwenyekiti wa BMT, Leodegar Tenga

Rais wa Fifa Gianny Infatinho (Kushoto) akiwa na waziri mkuu, Kassim Majaliwa leo

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI