MASIKINI HIMID MAO, KUKAA NJE WIKI SITA

Na Alex Jonathan. Dar es Salaam

Kiungo wa mabingwa wa kombe la Mapinduzi, Azam Fc Himid Mao Mkami atalazimika kukaa nje kwa kipindi cha wiki sita kuuguza majeraha baada ya kufanyiwa upasuaji nchini Afrika Kusini, kiungo huyo alianza kukosekana katika michezo kadhaa ya timu yake ya Azam Fc na kupelekea kuyumba kwa kikosi hicho.

Mao ambaye anafahamika kwa jina la Ninja kutokana na uchezaji wake, aliumia akiwa na kikosi hicho na alishindwa kuendelea kuichezea timu hiyo ambayo imempa majukumu ya unahodha.

Azam Fc mpaka sasa inashikilia nafasi ya tatu ikiwa na pointi 35 huku ikishuka uwanjani mara 19, kikosi hicho kitaumana na KMC siku ya Jumamosi katika michuano ya Azam Sports Federation Cup hatua ya 16 Bora

Himid Mao atakaa nje kwa muda wa wiki sita

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI