SINGIDA UNITED YAFUFUKIA KWA PRISONS

Na Mwandishi Wetu. Singida

Wenyeji Singida United jioni ya leo wameamka usingizini baada ya kuichakaza Tanzania Prisons bao 1-0 mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara uliopigwa uwanja wa Namfua Singida.

Goli ambalo limeibeba Singida United limefungwa na mshambuliaji wake Mzambia Elinyesia Sumbi na kuifanya timu hiyo kukwea hadi nafasi ya nne.

Vijana wa Singida United wanaonolewa na Mholanzi Hans Van der Pluijm wamefikisha pointi 27 wakiwa nyuma ya Yanga yenye pointi 28, Singida sasa inajiandaa kucheza na Mwadui hapo hapo Namfua mwishoni mwa wiki ijayo

Singida United imeilaza Prisons leo

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI