Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Simba yaihofia Azam, yataka mechi yake isogezwe mbele

Na Ikram Khamees. Dar es Salaam

Vinara wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Simba Sc imeanza kuingia mchecheto baada ya kuitaka Bodi ya Ligi (TPLB) kuisogeza mbele mechi yake dhidi ya Azam Sc itakayochezwa Februali 11 mwaka huu.

Akizungumza jana, Mkuu wa kitengo cha habari na mawasiliano wa klabu hiyo, Haji Sunday Manara amesema ratiba yao inawapa ugumu kidogo kwani kwa sasa akili zao wanazielekeza kwenye michuano ya kimataifa ambapo Simba itacheza na Wadjibout.

Manara amedai ratiba ya Ligi Kuu Bara inawabana kwani Simba itacheza na Ruvu Shooting Februali 4 kisha na Azam Fc halafu itaenda Shinyanga kucheza na Mwadui kabla ya kucheza kombe la Shirikisho barani Afrika.

Manara amedai mipango ya Simba ni kufika mbali katika michuano ya Afrika na ndio maana wamemchukua kocha Mfaransa, Pierre Lechantre ambaye amewahi kuipa ubingwa wa Afcon, Cameroon mwaka 2000.

Kwa maelezo ya Manara, Simba wanaiomba Bodi ya Ligi iwasogezee mbele mchezo wao dhidi ya Azam ikiamini itajipanga vizuri, lakini ni sawa kama inaigwaya kwani timu hizo zilipokutana hivi karibuni katika michuano ya kombe la Mapinduzi huko Zanzibar, Simba ilifungwa bao 1-0 hivyo imeingia hofu

Haji Manara Afisa habari wa Simba Sc

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa