Mashabiki Yanga wamkumbuka Mwambusi

Na Saida Salum. Dar es Salaam
Kufuatia kiwango kibovu inachokionyesha Yanga kwa sasa, baadhi ya mashabiki wa klabu hiyo wamemkumbuka aliyekuwa kocha msaidizi Juma Mwambusi wakidai ni bora yeye kuliko Shadrack Nsajigwa.
Wakizungumza tofauti kupitia mitandao ya kijamii, mashabiki hao wameelezea hisia zao na kudai kwa sasa Yanga haiwapi raha kwani soka wanalocheza haliwavutii na timu yao inazidi kuwapa presha.
Wanadai Yanga inacheza soka ambalo hawajazoea kuliona kwani hata ushindi wake umekuwa wa bahati, Yanga iliifunga Ruvu Shooting bao 1-0 uwanja wa Taifa Dar es Salaam lakini Ruvu ndio waliutawala mchezo huo.
Hivyo wameutaka uongozi wa Yanga kumrejesha haraka kocha msaidizi Juma Mwambusi ambaye amejiuzuru ili aweze kuinusuru timu yao, kwani Mwambusi amefanya vizuri alipohudumu kwenye nafasi hiyo

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI