Man United klabu tajiri duniani

Manchester United imeongoza orodha ya klabu 20 tajiri zaidi duniani kwa mwaka wa pili mfululizo na mara ya 10 kwa jumla , kulingana na kampuni ya Deloitte.
Mbali na msimu wa 2016-17 jumla ya mapato ya klabu hizo 20 imeongezeka kwa asilimia 6 hadi €7.9bn (£6.97bn), ikiwa ni rekodi mpya.
Real Madrid ilioongoza kwa miaka 11 ilikuwa ya pili na Barcelona ikawa ya tatu.
Kulikuwa na rekodi ya klabu 10 za Uingereza katika orodha hiyo ya 20 bora.
Orodha hiyo inaangazia mapato yaliopatikana na haiangazii madeni ya vilabu.
•1. Manchester United: €676.3m
•2. Real Madrid: €674.6m
•3. Barcelona: €648.3m
•4. Bayern Munich; €587.8m
•5. Manchester City: €527.7m
•6. Arsenal: €487.6m
•7. Paris Saint Germain: €486.2m
•8. Chelsea: €428m
•9. Liverpool: €424.2m
•10. Juventus: €405.7m
Duru: Deloitte, Mapato ya msimu wa  2016-17

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI