Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KUSUJUDU KWA GADIEL MICHAEL KWAZUA MSHANGAO, MWENYEWE AFAFANUA

Na Saida Salum. Dar es Salaam

Madhabiki wa soka nchini jana waliingia na mshangao kufuatia beki wa pembeni wa mabingwa wa soka nchini, Yanga Sc, Gadiel Michael Mbaga kushangilia bao lake kwa kusujudu kama waislamu.

Beki huyo wa upande wa kulia aliyesajiliwa na Yanga mwanzoni mwa msimu huu akitokea Azam Fc, jana aliifungia Yanga bao la ushindi dhidi ya Azam Fc katika uwanja wa Azam Complex, Chamazi.

Katika mchezo huo Yanga ilishinda mabao 2-1 na Azam Fc walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa dakika ya 3 kipindi cha kwanza na Shabani Chilunda, lakini Obrey Chirwa akaisawazishia Yanga kabla ya Gadiel kufunga la pili na la ushindi.

Baada ya kufunga, Gadiel alikimbia pembeni na kuinama chini akiswali kwa mtindo wa kusujudu ambao unatumiwa sana na waumini wa dini ya Kiislamu, baada ya kufanya hivyo mashabiki wa soka walishangazwa huku wengine wakidai mchezaji huyo ni Muislamu na wengine wakidai hata Wakristo hufanya hivyo.

Lakini baadaye Gadiel alitolea ufafanuzi kuwa aliamua kusujudu akiwasalimia viongozi wa Azam Fc ambao alifanya nao kazi vizuri lakini walimzuia asijiunge na Yanga na walitaka akae nje mpaka mkataba wake uishe hivyo amewaonyesha kitu kwa kufunga bao la kistadi

Gadiel Michael amebebwa juu na Obrey Chirwa wakishangilia jana

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa