KAGERA SUGAR VS SIMBA NI MECHI YA KISASI

Na Paskal Beatus. Bukoba

Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inaendelea tena leo kwa kuzikutanisha Kagera Sugar na Simba Sc katika uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.

Huo ni mchezo wa kisasi kutokana na kumbukumbu ya msimu uliopita ambapo Simba ililala 2-1 mpaka kuamua kukata rufaa TFF kisha kutishia kwenda Fifa kwa kile kilichodaiwa Kagera Sugar kumchezesha Mohamed Fakhi aliyekuwa na kadi tatu za njano.

Kwa maana hiyo mechi ya leo itakuwa ya kisasi, Simba ikitaka kulipiza kisasi, lakini pia itakuwa mechi ya uhasama kwani inawakutanisha tena Juma Nyosso na John Bocco ambao walikuwa maadui hawapatani na hasa Nyosso alimtomasa makalioni Bocco hivyo hatujui leo kitatokea kitu gani Kaitaba, Simba ikishinda ama kutoka sare itarejea kileleni

Kagera Sugar inaumana na Simba leo

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI