ISMAIL SUMA AZIKWA BURUNDI

Na Mwandishi Wetu.
Mlinda mlango wa zamani wa kimataifa wa Tanzania, Ismail Suma amezikwa jana mjini Bujumbura, Burundi baada ya familia yake kushindwa kuusafirisha mwili nchini Tanzania.
Suma aliyezichezea Kariakoo Lindi, Yanga, Simba na African Lyon, amezikwa jana katika makaburi ya Bujumbura, Burundi kufuatia kufariki dunia kwa maradhi Ini.
Kipa huyo aliondoka Tanzania na kwenda DR Congo kucheza soka la kulipwa ambapo pia aliondoka na kuelekea Burundi pia kucheza soka la kulipwa ambapo mauti yakamfika.
Baadhi ya wachezaji wenzake aliocheza nao nchini Tanzania wameonyesha kusikitishwa na kifo cha kipa huyo na kuliomba Shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) kusaidia kuuleta mwili nyumbani Tanzania kwa mazishi

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI