AUBAMEYANG KUTUA ARSENAL

Klabu ya Arsenal inataka kumnunua Pierre Emerick Aubameyang raia wa Gabon kwa kitita cha e60 m, kutoka kwa klabu ya Borrusia Dortmund ya Ujeruman.

Aubameyang (28) ameishawishi Arsenal ambayo hivi karibuni iliondokewa na mshambulizi wake Alexis Sanchez raia wa Chile aliyejiunga na Manchester United.

Sanchez alipishana na Henrick Mkhitaryan ambaye amejiunga na washika bunduki hao wa Amirates, ujio wa Aubameyang hautakuwa rahisi kwani Dortmund hawatamruhusu mpaka pale itakapofanikiwa kumnasa straika mwingine hatari lakini kuna uwezekano wa Olivier Giroud akaangukia kwao

Pierre Emerik Aubameyang (Kushoto) yuko mbioni kujiunga na Arsenal

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI