Kagera Sugar yatuma salamu kombe la FA

Na Paskal Beatus. Bukoba

Timu ya Kagera Sugar ya Bukoba jana ilifanikiwa kuingia hatua ya 32 bora ya michuano ya Azam Sports Federation Cup, maarufu kombe la FA baada ya kuichakaza timu ya Makambako mabao 7-0 uwanja wa Kaitaba, Bukoba.

Mshambuliaji wake mkongwe Themi Felix "Mnyama" aligeuka shujaa baada ya kufunga magoli matatu peke yake (Hat trick) huku Peter Mwalyanzi akifanikiwa kufunga magoli mawili na Venance Ludovic na Mwahita Salehe wakifunga goli moja kila mmoja.

Kwa ushindi huo mkubwa kabisa ilioupata Kagera Sugar ni kama salamu kwa mabingwa watetezi Simba SC ambao leo wanashuka uwanja wa Azam Complex, Chamazi mjini Dar es Salaam kuanza kutetea taji lake huku wakiwaza makali ya Kagera Sugar

Themi Felix (Kulia) amefunga magoli matatu jana

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI