Waziri Mwakyembe azuia Simba kukabidhiwa kwa mwekezaji Jumapili

Na Mwandishi Wetu. Dar es Salaam

Waziri wa habari, michezo, sanaa na utamaduni, Dk Harrison Mwakyembe, amesema kwa mujibu wa sheria za jamuhuri ya muungano wa Tanzania, hairuhusu klabu yoyote ya michezo inayomilikiwa na wanachama kuuza Hisa kwa asilimia zaidi ya 49.

Mwakyembe ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumza na chombo kimoja cha habari ambapo amefafanua kuwa klabu inayomilikiwa na mtu binafsi ndiyo inaruhusiwa kuuza hisa zaidi ya 49 na kumilikiwa na mwekezaji.

Kwa maana hiyo Mwakyembe amezuia mchakato wa kumkabidhi mwekezaji aliyeshinda zabuni ya kununua Hisa asilimia 50 za klabu ya Simba, ambapo Jumapili ya Desemba 3 itamtambulisha kwa wanachama na kupewa klabu aiendeshe.

Waziri Mwakyembe amezuia Simba isiuzwe kwa asilimia 50

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Kocha Simba anataka wachezaji wapya watano

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI