Simba kuwateketeza Lipuli leo

Na Ikram Khamees. Dar es Salaam

Vinara wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara, Simba SC, jioni ya leo inawakaribisha "Wanapaluhengo", Lipuli FC kutoka mkoani Iringa, mchezo wa Ligi Kuu bara katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Simba ambao ni vinara wa ligi hiyo wakiwa na pointi 22 sawa na Azam isipokuwa wana mabao mengi ya kufunga, watajihakikishia kukaa kileleni leo endapo watailaza timu hiyo inayonolewa na mchezaji na kocha wa zamani wa Simba, Seleman Matola.

Hata hivyo Lipuli inajivunia kwa kikosi bora na Simba inatakiwa isiwadharau Lipuli kwani lolote linaweza kutokea.

Simba itaiteketeza Lipuli leo

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI