Bocco asema ataendeleza kufunga

Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam

Mshambuliaji wa vinara wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara, Simba SC, John Bocco "Adebayor" amesema ataendeleza moto wake wa kufunga kila mchezo kama alivyofanya dhidi ya Tanzania Prisons mwishoni mwa wiki iliyopita.

Akizungumza na Mambo Uwanjani, Bocco amesema amepania kuingia katika orodha ya wanaowania kiatu cha dhahabu kwa kufunga kwani uwezo anao na ameshawahi kufanya hivyo, mshambuliaji huyo aliifungia Simba goli pekee la ushindi na kuifanya iendelee kusimama kileleni mwa msimamo wa ligi kwakufikisha pointi 22.

Mshambuliaji huyo kwa sasa amefunga jumla ya magoli mawili na yote amefunga kiustadi mkubwa, Bocco ameahidi kufunga katika michezo inayofuatia ambapo Simba itacheza na Lipuli Jumapili katika uwanja wa Azam Complex, Chamazi

John Bocco ameahidi kuendeleza moto wake wa kufunga

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI