YANGA YAIENDEA SIMBA, MORO

Na Ikram Khamees. Morogoro

Klabu bingwa ya soka Tanzania bara, Yanga SC imeingia kambini rasmi jana mjini Morogoro ikiwa tayari kabisa kuchuana na mahasimu wao Simba SC, Jumamosi ijayo uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Msemaji wa Yanga, Dissmas Ten amethibitisha kikosi hicho kuwasili jana Morogoro kikitokea Shinyanga na basi lake, hata hivyo Ten amedai wavhezaji wake watatu ambao iliwaacha Dar es Salaam kwa maana Amissi Tambwe, Donald Ngoma na Thabani Kamusoko nao wameungana na wenzao kambini hapo.

Yanga yenye pointi 15 na mechi saba sawa na mahasimu wake Simba SC ambao wako kileleni kwa tofauti ya magoli ya kufunga, itangia uwanjani ikitaka kulipiza kisasi baada ya kufungwa kwa mikwaju ya penalti katika mchezo wa Ngao ya Jamii uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Agosti 23 mwaka huu

Kikosi cha Yanga kimeingia kambini jana mjini Morogoro

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI