Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MTIBWA SUGAR KURUDI KILELENI LEO?

Na Ikram Khamees. Morogoro

Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara inaendelea tena kwa nyasi za viwanja sita kuwaka moto baada ya juzi na jana kufanyika mechi moja moja, Katika uwanja wa Manungu Complex mjini Morogoro shughuri itakuwa pevu pale Mtibwa Sugar itakapowaalika Singida United.

Mchezo huo licha kwamba utakuwa mgumu lakini rekodi zinaibeba Mtibwa Sugar inayonolewa na mwanasoka wake wa zamani, Zuberi Katwila kuibuka na ushindi na kukamata usukani, Mtibwa ina pointi 15 kwa mechi 7 hivyo ikishinda itafikisha pointi 18 itaziacha Simba, Yanga na Azam zenye pointi 16 kila moja.

Simba na Yanga jana zilishindwa kutambiana Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam baada ya kumaliza dakika 90 zikitoka sare ya 1-1, na juzi Azam FC iliifunga Mbeya City bao 1-0 katika uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi.

Mechi nyingine tano zitapigwa leo ambapo Majimaji itawaalika Mwadui FC, uwanja wa Majimaji Songea, Kagera Sugar na Ndanda zitaumana Kaitaba pale Bukoba, Tanzania Prisons na Ruvu Shooting, Sokoine Mbeya, Lipuli FC na Mbao FC, Samora mjini Iringa wakati Njombe Mji FC itakapowaalika Stand United pale Sabasaba Stadium, Njombe

Kikosi cha Mtibwa Sugar kinarejea kieleni leo

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa