TID kugombea Ubunge mwaka 2020

Na Saida Salum. Dar es Salaam

Mwanamuziki maarufu wa Bongofleva, Khalid Mohamed "TID" amesema atawania ubunge ifikapo mwaka 2020 endapo atapata ridhaa kutoka kwa wazee.

TID ameyasema hayo asubuhi ya leo akihojiwa na Efm ambapo amedai atagombea nafasi hiyo endapo wazee watampa baraka zote, TID amedai atagombea ubunge katika jimbo la Kinondoni ambapo ndipo anapoishi.

Msanii huyo aliyepata kutamba na nyimbo mbalimbali ikiwemo "Zeze", "Siamini" na nyinginezo, amewahi kutuhumiwa madawa ya kulevya na alikamatwa katikati ya mwaka huu na kufunguliwa mashitaka na serikali kuhusu matumizi ya dawa hizo yeye na wasanii wenzake

TID atagombea Ubunge mwaka 2020

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI