Mzee Akilimali asema, Clement Sanga anaihujumu Yanga

Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam

Katibu wa Baraza la wazee la klabu ya Yanga, mzee Ibrahim Akilimali amesema kwamba, makamu kaimu mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga anaihujumu timu hiyo isifanye vizuri katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu huu.

Akilimali ameyasema leo katika kipindi cha michezo cha Efm asubuhi, amedai Sanga amejiweka pembeni wakati timu ikiwa katika kipindi kigumu inachopitia.

Amedai kiongozi huyo anataka kuona Yanga inashuka daraja ili lawama zote abebeshwe mzee Akilimali ambaye alimkataa Manji na sera yake ya kuikodisha Yanga.

Katibu wa Baraza la wazee la Yanga,mxee Ibrahim  Akilimali

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI