TANZANIA YATINGA ROBO FAINALI COSAFA CUP

Na Exipedito Mataruma. Rustenburg.

Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars imefanikiwa kuingia robo fainali ya michuano ya Mataifa ya ukanda wa kusini mwa Afrika, Cosafa Castle Cup baada ya kutoka sare ya kufungana bao 1-1 na Mauritius.

Mchezo huo uliokuwa mkali na wa kuvutia, Stars ilisawazisha bao kupitia kwa winga wake Simon Msuva aliyeingia kipindi cha pili.

Kwa matokeo hayo Tanzania inaungana na Botswana, Zambia, Namibia, Lesotho, Swaziland na Afrika Kusini kucheza robo fainali huku zikisubiria timu nyingine moja kutoka kundi B.

Katika mchezo mwingine wa kundi A, Angola ililazimishwa suluhu 0-0 na Malawi na kuifanya Tanzania isonge hatua nyingine kirahisi, Stars itakutana na mwenyeji Afrika Kusini, Bafana Bafana

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI