Tambwe asaini miaka miwili Yanga

Na Ikram Khamees. Dar es Salaam

Mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga SC wamezidi kuendelea kuwabakiza nyota wake baada ya usiku huu kuthibitisha kumuongezea mkataba wa miaka miwili mshambuliaji wake Amissi Jocelyin Tambwe.

Tambwe aliyejiunga na mabingwa hao misimu miwili iliyopita akitokea kwa mahasimu Simba, amesaini mkataba mpya leo ambao utamfanya aendelee kusalia hapo hadi mwaka 2019.

Msimu wake wa kwanza Tambwe amekuwa mfungaji bora akifikisha mabao 21 na vilevile bado amekuwa katika kiwango kizuri na kufikia Yanga kunogewa naye na kumuongezea mkataba

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI