STARS YAKOMAA KILELENI SAUZI

Na Exipeditor Mataruma. Afrika Kusini.

Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars imeilazimisha sare tasa 0-0 dhidi ya Angola mchezo wa kundi A michuano ya Cosafa Castle Cup Uwanja wa Royal Bafokeng mjini Rustenburg, Afrika Kusini.

Mechi hiyo ilipigwa usiku kuanzia saa 2:30 ilishuhudiwa kiungo wake Muzamiru Yassin Selembe akiibuka Man of the Match akionyesha kiwango kikubwa.

Kwa maana hiyo Stars imefikisha pointi 4 ikiongoza kundi A kwa wingi wa mabao dhidi ya Angola ambao nao wana pointi 4 kama Stars ila wao wana bao moja wakati Stars inayo mawili, keshokutwa Stars itacheza na Mauritius mechi ikipigwa jioni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI