Ni vita ya Tanzania na Angola leo

Na Exipedito Mataruma. Afrika Kusini.

Kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, jioni ya leo kitashuka uwanjani kwa mara ya pili kukwaruzana na Angola katika mchezo wa michuano ya kombe la COSAFA Castle Cup.

Tanzania inahitaji ushindi katika mchezo huo ili iweze kutinga robo fainali ya michuano hiyo inayoshirikisha mataifa 13, Tanzania ikishiriki kama nchi mwalikwa, ilianza vema katika fainali hizo baada ya kuilaza Malawi mabao 2-0.

Mabao yote ya Tanzania yalifungwa na winga wake Shiza Kichuya, kuelekea katika mchezo wa jioni, kocha wa Tanzania Salum Mayanga amesema vijana wake wapo tayari kwa mchezo huo na amewaahidi Watanzania zawadi nzuri ya sikukuu ya Iddi El Fitr

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI