Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Toto wamebana wameachia, Tambwe awapa ndoo ya tatu Yanga

Na Salum Fikiri Jr. Dar es Salaam

Bao lililofungwa kunako dakika ya 81 na mshambuliaji Amissi Tambwe raia wa Burundi, jioni ya leo limetosha kabisa kuwapa ubingwa wa tatu mfululizo Yanga SC dhidi ya watoto wao Toto Africans.

Mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kwa ushindi wake wa 1-0 umeifanya Yanga ifikishe pointi 68 na michezo 29 sawa na vilabu vyotw vinavyoshiriki ligi hiyo.

Haikuwa kazi rahisi kwa Yanga kujipatia bao la ushindi kwani vijana wa Toto Africans "Wana Kishamapanda" leo walistahili pongezi kwa kuwabana vilivyo baba zao Yanga SC na kuwalazimisha suluhu ya 0-0 hadi mapumziko.

Kipindi cha pili pia kilikuwa kigumu kwa Yanga kwani mabeki wa Toto walifanya kazi ya ziada kuwazuia washambuliaji wa Yanga wakiongozwa na Obrey Chirwa wasifanye madhara langoni mwao, Kipa wa Toto David Kisu leo alikuwa kikwazo kwa Yanga kwa kuokoa magoli kadhaa.

Mabadiliko yaliyofanywa na Yanga ya kumtoa Geofrey Mwashiuya na kumwingiza Emmanuel Martin viliisaidia sana Yanga kwani dakika ya 36 ya kipindi cha pili Amissi Tambwe aliipatia Yanga bao la ushindi ambalo linaelekea kuishusha daraja Toto.

Yanga watabakiwa na mchezo mmoja dhidi ya Mbao FC ambao utafanyika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, endapo Yanga itapoteza mchezo huo bado inaweza kuwa mabingwa kwani wapinzani wao kwenye mbio za ubingwa Simba SC wanaweza kuzifikia pointi 68 walizonazo Yanga lakini tofauti yao ni mabao ya kufunga na kufungwa

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa