Simba yaua Polisi Dodoma 3-0

Na Saida Salum. Dodoma

Simba SC wameendelea kuwapa raha mashabiki wake baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya wenyeji Polisi Dodoma uwanja wa Jamhuri mjini hapa.

Mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi Laudit Mavugo ameendelea kuwatesa makipa wa Tanzania baada ya kufunga bao la kwanza katika mchezo huo wa kirafiki jioni ya leo.

Dakika 45 za kwanza zilimalizika Simba wakiwa mbele kwa bao moja, lakini kipindi cha pili wakaongeza mabao mawili kupitia kwa winga wake machachari Shiza Ramadhan Kichuya kwa penalti na mshambuliaji Juma Luizio Ndanda akafunga la tatu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Kocha Simba anataka wachezaji wapya watano

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI