Jeshi la Azam mguu sawa Swaziland

Na Mrisho Hassan. Mbabane

Kikosi cha Azam FC kesho kinajitupa uwanjani kurudiana na Mbabane Swallors ya Swaziland mchezo wa hatua ya 32 bora ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika.

Azam FC inaingia uwanjani ikiwa na mtaji wa bao moja ililolipata Uwanja wa Azam Complex zilipokutana katika mchezo wa mkondo wa kwanza.

Mchezo wa kesho Azam inahitaji sare ya aina yoyote na ikivuka kigingi hicho itaumana na moja kati ya timu zilizoondolewa kwenye Ligi ya mabingwa Barani Afrika, Azam itamtegwmea zaidi winga Ramadhan Singano ambaye ndiye aliyefunga bao katika mchezo wa kwanza

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI