Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Ni mechi ya kisasi Simba Vs Azam

Na Ikram Khamees, Dar es Salaam

Leo ndio leo asiye na mwana abebe jiwe, vinara wa Ligi Kuu Bara Simba SC jioni ya leo wanashuka uwanja wa Taifa Dar es Salaam kukwaruzana na Azam FC mchezo wa Ligi Kuu Bara unaotazamiwa kuwa mkali.

Mchezo huo utakuwa mkali kutokana na miamba hiyo kutoka kuumana hivi karibuni katika fainali ya kombe la Mapinduzi iliyofanyika Uwanja wa Amaan Zanzibar na Azam kushinda 1-0.

Simba wanaingia katika mchezo huo wa marudiano wa Ligi Kuu lakini wakitaka kulipiza kisasi baada ya kulala kwenye fainali, kwa upande wa Azam nao wanataka kushinda mchezo huo ili kulipiza kisasi kwani katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu Bara walilala 1-0.

Azam itawategemea zaidi nyota wake John Bocco 'Adebayor', Salum Abubakar, Himid Mao Mkami, Yahaya Mohamed na Stephano Kingue Mpongou, Simba nao watamtegemea zaidi Shiza Kichuya, Ibrahim Ajibu, Mohamed Ibrahim, Mzamiru Yassin na Laudit Mavugo.

Endapo Simba itashinda mchezo huo itaendelea kukalia usukani kwa kufikisha pointi 47 na kama ikifungwa ama kutoka sare basi Yanga anaweza kukamata usukani endapo kesho ataifunga Mwadui

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa