Simba yamuuza kinyemela Danny Lyanga

Na Mrisho Hassan, Dar es Salaam

Klabu ya Simba ya Dar es Salaam, inadaiwa imemuuza mshambuliaji wake Danny Lyanga kwa klabu ya Oman SC ya Oman inayoshiriki Ligi kuu nchini humo.

Hata hivyo, Mtendaji mkuu wa Wekundu hao wa Msimbazi, Patrick Kahemela amekataa vikali kuthibitisha hilo na kudai Lyanga hajauzwa isipokuwa ameenda Oman kufanya majaribio ma kama akikubalika anaweza kuuzwa.

Lakini mshambuliaji huyo aliondoka mwezi uliopita kujiunga na timu hiyo na sasa ni mchezaji wa Oman SC lakini haijulikani kama amesaini mkataba wa muda gani huku ikidaiwa Simba ilimuuza kinyemela.

Lyanga ni mmoja kati ya washambuliaji hatari waliofanya vizuri msimu uliopita akiwa na Simba  sambamba na Ibrahim Ajibu, Hamisi Kiiza na wengineo

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI