Simba kusahihisha makosa kwa Ruvu Shooting leo?

Saida Salum, Dar es Salaam

Wekundu wa Msimbazi, Simba SC, jioni ya leo wanashuka uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam kuwakabili Ruvu Shooting ya Mlandizi mkoani Pwani mchezo wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara.

Simba wanataka kusahihisha makosa yao kwani katika mchezo wao dhidi ya JKT Ruvu walilazimishwa sare tasa ya 0-0 hivyo leo hawatakubali kulazimishwa tena sare.

Ikiwa chini ya washambuliaji wake Laudit Mavugo raia wa Burundi, Fredrick Blagnon raia wa Ivory Coast na Ibrahim Ajibu 'Kadabla' kwa vyovyote wataondoka na pointi tatu.

Nao Ruvu Shooting ya Masau Bwire nayo itamtegemea zaidi kiungo wake mkongwe Shaaban Kisiga 'Marlone' ambaye aliwahi kuichezea Simba katika misimu kadhaa iliyopita

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI