Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mwaisabula afichua ya Serengeti Boys

Na Prince Hoza, Dar es Salaam

Kocha wa zamani wa Bandari Mtwara, Ashanti na Yanga SC, Kenny Mwaisabula 'Mzazi' amefichua ya Serengeti Boys ya kutumia wachezaji vijeba mwaka 2004 na kuondoshwa na CAF kwenye fainali za mataifa Afrika zilizofanyika Gambia.

Akizungumza katika kipindi cha michezo cha MBS kinachorushwa kuanzia saa tano asubuhi mpaka saa saba mchana na redio Sibuka ya jijini Dar es Salaam, Mwaisabula amesema Serengeti timu ya umri wa miaka 17 lakini ilikusanya wachezaji waliozidi umri huo.

Mzazi aliwataja wachezaji kama Athuman Idd 'Chuji' , Mrisho Ngasa, Kiggy Makassy, Amir Maftah, Hassan Bwaza, Patrick Mangunguli, Nizar Khalfan, Nurdin Bakari, Yusuph Mgwao na David Mwantebe tayari walishazidi umri huo kwakuwa walianza kucheza Ligi kuu kabla hawaitwa timu hiyo ya vijana.

Mbali na Nurdin kugundulika, bado kulikuwa na wachezaji wengine anaowafahamu kudanganya umri ni wengi akiwemo Chuji na Mangunguli, 'Chuji alikuwa anaichezea Polisi Dodoma halafu akaitwa Serengeti, ina maana alianza kucheza Ligi kuu akiwa na miaka 16? mbona akuandikwa kwenye kitabu cha Guinnes kama mchezaji mdogo zaidi', anasema Mzazi ambaye kwa sasa ni mchambuzi.

Aidha kocha huyo wa zamani wa Yanga amesema hadi sasa hakuna mchezaji mwenye miaka 17 katika kikosi cha Serengeti Boys na wale waliopo ni wakubwa, amedai kwa sasa kuna uhaba wa wachezaji wenye umri kama huo kutokana na mazingira yenyewe huku akilalamikia ukosefu wa viwanja

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa