DANGOTE KUIMWAGIA MAPESA NDANDA FC

Na Saida Salum, MTWARA

BILIONEA Aliko Dangote raia wa Nigeria anatajwa kuwekeza kwenye timu ya ligi kuu ya Ndanda Fc ya mjini hapa, endapo bilionea huyo namba moja barani Afrika atawekeza kwenye timu hiyo basi tutegemee mabadiliko makubwa.

Habari ambazo bado hazijathibitishwa zinasema bilionea huyo mwenye viwanda vya kutengeneza Cement ya aina yake ya Dangote inayouzwa kwa gharama nafuu.

Bilionea anatajwa kuichukua timu hiyo kama mdhamini hivyo kutawafanya Ndanda kuogelea manoti, hii ni mara ya pili kwa Ndanda kupata wafadhili kwani tayari ilishaonja noti za mfanyabiashara wa matairi Nassoro Binslum ambaye hata hivyo ameachana na Ndanda

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI