ALI KIBA AINGIA ANGA ZA CHRIS BROWN

MSANII wa muziki wa bongofleva Ali Kiba leo akiwa nchini Afrika Kusini amesaini mkataba mkubwa na kampuni ya SONY MUSIC ambayo pia inafanya kazi na wasanii wakubwa kama Chris Brown, Davido na John Legend.

Kiba aliyeachia wimbo wake mpya 'Aje' aliondoka jana kuelekea 'Bondeni' kwa Jacob Zuma na leo ameweka historia mpya kwenye tasnia ya muziki Tanzania.

Msanii huyo sasa atafanya kazi chini ya usimamizi wa kampuni hiyo kubwa ambayo imeshawasaidia wanamuziki mbalimbali duniani kutambulika

Ali Kiba akiwa anashikana mikono na mmoja wa mabosi wa Sony Music leo nchini Afrika Kusini

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI