Ruka hadi kwenye maudhui makuu

YANGA YAFA KISHUJAA LIGI YA MABINGWA AFRIKA, YAPIGWA 2-1 YAANGUKIA SHIRIKISHO

Na Exipedito Mataruma, ALEXANDRIA

MABINGWA wa Tanzania bara Yanga Sc wameondoshwa katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika bada ya kufungwa kishujaa mabao 2-1 na Al Ahly ya Misri mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa Borg Al Arab mjini Alexandria usiku ya Jumatano.

Katika mchezo huo Yanga ilixheza vizuri muda wote na kulisakama lango la Al Ahly kiasi kwamba mwamuzi wa mchezo huo alipopuliza kipyenga kuashiria mpira umemalizika mashabiki wa Al Ahly walishangilia kama wametwaa ubingwa wa Afrika.

Kwa sasa unaweza kutamka kuwa Yanga na Al Ahly ni kama wapinzani wa jadi katika soka la Afrika kutokana na ushindani ulioonyeshwa usiku huu, Al Ahly walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Hossam Ghaly.

Bao lilipatikana kipindi cha pili dakika ya 52 baada ya kuunganisha kwa kichwa kona ya Ahmed Fathi, Yanga walitulia na kucheza soka la kitabuni na kufanikiwa kusawazisha bao hilo kupitia mshambuliaji wake Mzimbabwr Donald Ngoma kufuatia kazi nzuri iliyofanywa na Juma Abdul.

Goli hilo la kusawazisha lilipatikana dakika ya 57, wakati wengi wakiamini mchezo huo unaweza kumalizika kwa sare ya 1-1 hasa baada ya kwisha kwa dakika 90 za kawaida mwamuzi aliongeza dakika 5, hapo ndipo yalipotokea maajabu ya soka kwani Abdallah Saed aliukwamisha mpira kimiani na kuwaondosha Yanga mashindanoni.

Yanga sasa itaangukia kombe la Shirikisho barani Afrika ambapo ratiba yake inatarajia kupangwa Alhamisi, na huenda ikakutana na Esperance ya Tunisia katika mchezo ujao

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa