Ruka hadi kwenye maudhui makuu

STAA WETU: JUMA ABDUL JAFFARI, MPISHI WA GOLI LA NGOMA, WAARABU WAMZIMIA

Na Exipedito Mataruma, ALIYEKUWA MISRI.

JUMA Abdul Jaffari ukiongeza lingine Mnyamani ni jina linalochomoza kwa sasa kwenye medani ya soka hapa nchini na kwingineko.

Anacheza nafasi ya ulinzi wa pembenj hasa akimudu upande wa kulia na akisaidia kupandisha mashambulizi, Abdul amekuwa na uwezo mkubwa wa kusababisha mashambulizi na timu yake kung' ara.

Akiwa katika kikosi hicho cha mabingwa wa soka nchini Yanga Sc, Abdul ameisaidia hadi kukamata usukani wa ligi kuu na kuweka hai matumaini yake ya kutetea ubingwa wa bara.

Nyota huyo pia amekuwa mpigaji mzuri wa mipira iliyokufa kwa maaba faulo, Abdul amejaaliwa nguvu za miguu na amekuwa akipiga mashuti makali hatimaye kuifungia timu yake magoli.

Anakumbukwa kwa magoli yake ya mashuti moja dhidi ya Azam Fc, ambapo alisawazisha makosa yake baada ya kujifunga kisha akapanda na kupiga bunduki kali na kufunga la kusawazisha, katika mchezo huo timu hizo zenye ushindani zilifungana mabao 2-2.

Abdul pia akafunga bao lingine dhidi ya APR ya Rwanda mchezo wa ligi ya mabingwa uliofanyika mjini Kigali ambapo Yanga ilishinda mabao 2-1, goli lake likiisaidia kuivusha Yanga raundi ya pili ya michuano hiyo mikubwa na yenye ukwasi mkubwa wa fedha.

Nyota yake inazidi kung' ara licha kwamba kocha wa timu ya taifa, Taifa Stars Charles Boniface Mkwassa ameshindwa kumuona, Mkwassa amekuwa akimtumia zaidi Shomari Kapombe.

Lakini Abdul ni mmoja kati ya wachezaji bora kwa sasa Afrika mashariki, beki huyo amekuwa katika kiwango cha juu mno na kuipa nguvu Yanga, Abdul alisajiliwa na Yanga misimu mitatu iliyopita akitokea Mtibwa Sugar ya Morogoro ambayo yenyewe ilimchukua toka Toto Africans ya Mwanza.

Tayari beki huyo ameshampoteza kabisa Mnyarwanda Mbuyu Twite ambaye alikuwa akianzishwa namba mbili, kasi ya Abdul imemfanya kocha wa Yanga Mholanzi Hans Van der Pluijm kumchezesha namba sita au tano.

WAARABU WAMTAMANI

Juma Abdul aliwashangaza Waarabu hasa wakati timu yake ya Yanga ilipocheza na Al Ahly mchezo wa marudiano ligi ya mabingwa barani Afrika hatua ya 16 bora uliofanyika uwanja wa Borg Al Arab mjini Alexandria.

Kwa bahati nzuri niliushuhudia kwa macho yangu kwa maana nilikuwepo uwanjani, Abdul ndiye mpishi wa bao la Yanga walilokipata dakika ya 57 lililofungwa na Mzimbabwe Donald Ngoma, lilikuwa goli zuri lakini lilitokana na jitihada binafsi za Abdul.

Mara baada ya kumalizika mchezo huo, mashabiki wa soka nchini Misri walifurahishwa naye huku wengine wakizitaka timu za Misri kumchukua.

Abdul alizaliwa Novemba 10 mwaka 1992 mjini Mwananyamala Dar es Salaam  na kuanza soka utotoni, nyota yake ilianza kuonekana tangia anacheza chandimu, Malengo yake ya baadaye  mara baada ya kuachana na Yanga ni kucheza soka la kulipwa ughaibuni.

Yanga wameshamuongezea mkataba mpya wa miaka miwili utakaomalizika mwaka 2018

Juma Abdul akipata maelekezo toka kwa kocha wake Hans Pluijm

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa