Ruka hadi kwenye maudhui makuu

STAA WETU: HASSAN KABUNDA, MTOTO WA NINJA WA YANGA ANAYEING' ARISHA MWADUI FC

Na Paskal Beatus, SHINYANGA

JINA la Hassan Kabunda linaonekana kama geni masikioni mwa watu, lakini wapo wanaomkunbuka beki wa zamani wa Tukuyu Stars, Yanga Sc na timu ya taifa ya Tanzania bara Kakakuona Salum Kabunda 'Ninja' ukipenda Msudan.

Beki huyo alijulikana kwa kucheza kibabe sana uwanjani mpaka ikafikia washambuliaji kuanza kumuogopa, Hassan Kabunda ni mtoto wa Salum Kabunda, lakini iko tofauti kidogo.

Hassan Kabunda yeye ni mshambuliaji na si beki kama ilivyokuwa kwa baba yake, kijana huyu amekuwa katika kiwango kizuri na kuwa msaada mkubwa kwenye timu yake ya Mwadui Fc ya Shinyanga.

Kabunda ni mshambuliaji wa timu hiyo na anakumbukwa vizuri hasa pale alipoifungia Mwadui mabao yote mawili dhidi ya Coastal Union mchezo wa ligi kuu bara Nwadui ikishinda ikishinda mabao 2-1.

Nyota huyo aliibukia katika mashindano ya Copa Cocacola akiwa na timu ya Mkoa wa Ilala, Kabunda akiwa na ndugu yake Ally Kabunda wote washambuliaji, walitamba katika michuano hiyo na baadaye wakasajiliwa na Ashanti inayoshiriki ligi Daraja la kwanza.

Kabunda amekuwa na uwezo mkubwa wa kutengeneza mashambulizi na anapokosekana uwanjani pengo lake linaonekana dhahili, mshambuliaji huyo anaichezea Mwadui Fc ya mjini hapa anbayo inanolewa na Jamhuri Kihwelu 'Julio'.

Umuhimu wake ulionekana katika mchezo wao wa ligi kuu bara dhidi ya mabingwa watetezi Yanga Sc uliopigwa uwanja wa Taifa Dar esvSalaam ambapo Yanga ilishinda 2-1, baada ya Mwadui kumtoa Kabunda na kumwingiza mkongwe Nizar Khalfan Yanga walionekana kupata ahueni kidogo.

Alipokuwepo uwanjani Kabunda, Yanga walishindwa kulifikia lango la Mwadui na matokeo yalikuwa 1-1 kipindi cha pili, lakini mabadiliko aliyoyafanya Julio ya kumtoa Kabunda yakawafanya Yanga wapande mbele na dakika ya 87 Haruna Niyonzima akaifungia Yanga bao la pili.

Kama mwalimu wa timu ya taifa, Taifa Stars Charles Boniface Mkwassa yatamulika vizuri basi kijana huyo anaweza kuwemo kwenye kikosi chake kwani ni miongoni mwa wachezaji wanaofaa kuitumikia

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa