Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MITANANGE MIWILI FA CUP KUPIGWA LEO, NANI KUCHEZA FAINALI

Na Ikram Khamees, DAR ES SALAAM

MICHUANO ya Azam Sports Federation Cup inatarajia kuendelea jioni ya leo katika viwanja viwili tofauti hatua ya Nusu fainali ambapo timu mbili zitafuzu fainali itakayopigwa mwezi Mei mwaka huu.

Tukianzia pambano linalosubiriwa kwa hamu kubwa na wapenzi wa soka katika miji ya Dar es Salaam na Tanga, mabingwa watetezi wa ligi kuu bara Yanga Sc watakuwa wageni wa Coastal Union ya Tanga uwanja wa CCM Mkwakwani.

Timu hizo zinakutana leo katika michuano hiyo inayofahamika zaidi kama FA Cup, Yanga inataka kulipiza kisasi kwani ilibutuliwa mabao 2-0 na vijana hao wa Wana Mangushi, Yanga ilifungwa kwenye mchezo huo wa ligi kuu bara.

Hivyo mchezo huo utakuwa mkali ikitaka kulipiza kisasi, pia ina machungu ya kutolewa kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika kwa kufungwa jumla ya mabao 3-2 na Al Ahly ya Misri, Coastal nao kwa sasa wako vizuri hasa baada ya kupata ushindi wa mara mbili mfululizo.

Coastal iliifunga Simba Sc mabao 2-1 mchezo wa Robo fainali ya FA Cup, pia ikaifunga JKT Ruvu bao 1-0 mchezo wa ligi kuu bara hivyo leo inataka kuendeleza ubabe kwa Yanga, tusubiri nini kitatokea.

Mjini Shinyanga katika uwanja wa Mwadui Complex, wenyeji Mwadui Fc itaialika Azam Fc ambao ni klabu bingwa Afrika mashariki, timu hizo zimekamiana vya kutosha katika Nusu fainali hiyo nyingine.

Kocha wa Mwadui Fc Jamhuri Kihwelu "Julio" amejitamba kumbwaga mzungu wa Azam Stewart Hall raia wa Uingereza, Azam nayo kama Yanga ina hasira ya kutolewa kwenye kombe la Shirikisho barani Afrika, Azam ilifungwa jumla ya mabao 4-2 na Esperance ya Tunisia.

Mwadui nao wana kumbukumbu mbaya ya kupoteza mechi mbili mfululizo za ligi kuu bara hivyo mchezo wa leo utakuwa mgumu na wakusisimua

Yanga Sc je watalipa kisasi?

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa