Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MICHANO: PHILIPO NYANDINDI "O TEN", ALISAHAU MSEMO HUU, UKIMUONA KOBE JUU YA MTI UJUE KAWEKWA

Na Mkola Man, TANGA

YAP....yap....yap Michano yangu ya leo inamchana Philipo Nyandindi "O Ten" kutoka mji kasoro bahari yaani Morogoro ila safari yake kimuziki ilianzia Upanga jijini Dar es Salaam katika kundi la East Coast Team.

Lakini kabla hajatua kundi hilo, O Ten alikuwa msanii wa kujitegemea huko Morogoro na siku moja wakati msanii Inspekta Haroun akitamba na 'Mtoto wa geti kali' alivutiwa na msanii huyo jukwaani na kuamua kumleta Dar es Salaam.

Inspekta ndiyo msanii wa kwanza kurekodi studio na O Ten wimbo unaojulikana kwa jina la "Siku za Hukumu ya mwisho'. na hapo ndipo safari ya O Ten ilipoanza.

KWANINI ALIINGIA EAST COAST

O Ten alijiunga na East Coast Team baada ya kutelekezwa na Inspekta ambaye alimuahidi kumsaidia kimuziki ndipo alipotua kundi hilo lililotamba sana, mwaka 2004 alitoka na nyimbo iitwayo 'Nicheki' iliyotengenezwa vizuri na prodyuza P Funk Majani iliyompa heshima ndani ya kundi lake na nje pia.

Kisha nyota yake ikaanza kung' ara na akajipatia mashabiki wengi na kuweka historia ya kufanya shoo na wapinzani wao TMK Wanaume Family katika ukumbi wa Bilicanas, kundi la East Coast lina wasanii maarufu kama King Crazy GK, Mwana FA, Pouline Zongo, Snare, Buff G, AY na O Ten mwenyewe.

Chakusikitisha sana kabla ajapata mafanikio akaanza malumbano na msanii mwenzake Afande Sele ambaye anatoka naye Morogoro akichukua muda mrefu East Coast Team ikavunjika na hapo ndipo ukawa mwisho wake licha kwamba alikongoja kidogo kwa kutoa wimbo "Akipendacho binti".

O Ten alisahau maneno ya waswahili ambayo yalitimia yanayosema ukimkuta kobe juu ya mti usishangae ujue amepandishwa, na O Ten hakuonekana tena mpaka leo, Yap Mkola Man naachia line, tukutane Ijumaa ijayo

Philipo Nyandindi "O Ten"

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa