CAF YAWAPA YANGA WAANGOLA

Na Exipedito Mataruma, CAIRO

SHIRIKISHO la kandanda barani Afrika CAF limeipangia klabu ya Yanga ya Tanzania kucheza na Segrada Esperance ya Angola (Pichani) mchezo wa kombe la Shirikisho barani Afrika.

Yanga na Esperance zimeangukia kombe la Shirikisho baada ya kuondoshwa kwenye ligi ya mabingwa Afrika, Yanga ilifungwa mabao 2-1 jana usiku na Al Ahly ya Misri uwanja wa Borg Al Arab mjini Alexandria.

Mechi za mchujo kombe la Shirikisho kuelekea kwenye makundi zinataraji kuchezwa kati Mei 6-7 na marudiano kuchezwa kati Mei 17-18, hiyo ni nafasi nyingine kwa Yanga kuandika rekodi kwani ikivuka hatua hiyo itaingia Robo fainali

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI