Ruka hadi kwenye maudhui makuu

STAA WETU: DONALD NDOMBO NGOMA: MSHAMBULIAJI ANAYEANZISHA MASHAMBULIZI MWENYEWE

Na Prince Hoza

Yanga leo jioni inashuka uwanja wa Taifa Dar es salaam kukabiliana vikali na APR ya Rwanda mchezo wa ligi ya mabingwa barani Afrika.

Katika mchezo huo utakaoanza saa kumi kamili jioni unatazamiwa kuwa mkali hasa kutokana na matokeo ya mchezo wa kwanza.

Yanga ilitangulia kushinda mabao 2-1 uwanja wa Amahoro mjini Kigali, shukrani kwa Juma Abdul na Thabani Kamusoko ambao ndio wauaji wa APR.

Lakini Yanga inajivunia mshambuliaji wake hatari Donald Ndombo Ngoma raia wa Zimbabwe, Ngoma aliyezaliwa Februali 4, 1989 mjini Halale Zimbabwe amekuwa katika kiwango cha juu mno tangia alipojiunga mwanzoni mwa msimu huu.

Ngoma alianza kushangaza wakati wa mchezo wake wa kwanza wa kombe la Kagame dhidi ya Gor Mahia ya Kenya mchezo uliopigwa uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Donald Ngoma alikuwa akiinyanyasa safu ya ulinzi ya Gor na kupelekea Yanga kujipatia bao la kuongoza lililofungwa naye, Ngoma alifunga goli hilo baada ya juhudi zake binafsi.

Utofauti mkubwa umeonekana kati ya mshambuliaji huyo na wengine waliopo hapa nchini ni mkubwa sana, Ngoma ni mshambuliaji nwenye uwezo mkubwa kwani anaweza kuanzisha mashambulizi yeye mwenyewe na pia akafunga.

Hadi sasa ameshafunga magoli 13 katika msimamo wa ligi kuu bara, lolote linaweza kutokea kwani anaweza kuibuka mfungaji bora mwisho wa siku.

Ngoma anakumbukwa vema na Simba kwani zilipokutana hivi karibuni  yeye ndiye aliyewalaza mapema mashabiki wa Simba, katika mchezo huo Yanga ilishinda mabao 2-0 huku yeye ni Amissi Tambwe wakifunga kila mmoja.

Yanga walifikia hatua ya kumsajili Ngoma baada ya kuridhishwa naye, Ngoma alikuwa akiichezea Fc Platinum ya Zimbabwe ambapo timu hiyo ilikutana mwaka jana na Yanga katika michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika.

Ndipo Yanga waliponogewa na soka lake na kuamua kumchukua, mshambuliaji ni mmoja kati ya washambuliaji hatari kabisa kuwahi kutokea hapa nchini na amekuwa akipigiwa hesabu za kuondoka nchini na kwenda kucheza soka la kulipwa ughaibuni

Changamoto nyingine anazopitia mshambuliaji huyo ni kuwindwa na mabeki wa timu pinzani, Ngoma anakaniwa sana na amekuwa akiongoza kwa kuchezewa rafu nyingi.

Hiyo inamfanya Ngoma kuwa na hasira kali na inafikia hatua anapaniki na kurudisha rafu anazochezewa, Ngoma kuna wakati anarusha ngumi na kusababisha kuonyeshwa kadi nyekundu.

Mara yavkwanza alikuwa akionyeshwa sana kadi lakini baada ya kocha wake Hans Van der Plujm kumkalisha kitako, Ngoma amebadilika na sasa arudishii rafu anazochezewa

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa