Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA YALIA NA YANGA, AZAM NA TFF

Na Saida Salum

Klabu ya Simba imeendelea kulalamikia ratiba ya ligi kuu bara inavyopanguliwa kila kukicha ikiwa na malengo ya kuzibeba Yanga na Azam.

Hajji Manara msemaji wa klabu hiyo ameishutumu TFF kwa kuonyesha waziwazi kuzibeba Yanga na Azam kwa kuziondolea mechi zake za ligi kuu bara hivyo sasa utakuwa mtihani mkubwa kwao.

Simba ibaongoza ligi hiyo kwa kukusanya pointi 54 lakini imeshuka dimbani mara 22 ikiwa ni tofauti ya mechi mbili na Yanga na mechi tatu na Azam.

Yanga ina pointi 50 wakati Azam ina pointi 47, kwahiyo kama itacheza na kushinda mechi zake tatu zilizosalia itafikisha pointi 56 na itakuwa imeishusha Simba katika nafasi yake ya kwanza.

Yanga nao wakishinda mechi zao mbili watafikisha pointi 56 na wataishusha Simba katika nafasi yake ya kwanza, Manara ameshangazwa na kitendo cha TFF kuzifutia Yanga na Azam mechi zake za ligi zilizopangwa kuchezwa hivi karibuni.

Msemaji huyo amedai hakuna ligi yoyote duniani inayosogezwa mbele kwa sababu kuna timu inashiriki michuano ya kimataifa, ameongeza kuwa hiyo ipo hapa Tanzania pekee na si kwingineko.

Hata hivyo Manara amedai hiyo ni mbeleko ya kuzibeba Yanga na Azam, Yanga haitacheza tena ligi mwezi huu na itasubiri hadi mwezi ujao, wakati Azam itacheza mchezo mmoja tu kisha itasubiri hadi mwezi ujao.

Simba itatelemka tena uwanjani siku ya jumamosi katika dimba la Mkwakwani Tanga kuwavaa Coastal Union ambao ni wababe wa Yanga na Azam, vigogo hivyo vyote vililala kwa Wagosi hao wa Kaya.

Yanga ilifungwa mabao 2-0 wakati Azam ilichapwa 1-0 na kuweza kutibua kasi yao ya kuelekea kwenye ubingwa

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa