Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MICHANO: HAWATOSHEKI NA UKUBWA WA MAJINA YAO, BADO WANAGOMBANIA MAJINA YA WANYAMA

Na Mkola Man, Tanga

Yap...yap...yap..Michano yangu ya leo inawachana chana na kupasua kuhusu kitendo cha wasanii watano wenye majina (Masupa staa) wakubwa ndani na nje ya bongo, wasanii hao kwakweli siwaelewi kabisa maana wanagombania majina ya wanyama wa porini.

Hivi karibuni wasanii watatu waligombania jina la mnyama Simba na kila mmoja akidai ni lake, wasanii hao ni Diamond Platinumz, Mr Blue na Afande Sele "Mfalme", wengine wawili wakigombania jina la Mamba.

Godfrey Tumaini maarufu Dudubaya na Shetta ama baba Kayla kila mmoja alikuwa akidai yeye ni mamba, wakati mamba wenyewe wanaishi majini na kamwe sijawahi kusikia au kuona mamba akiitwa Dudubaya au Shetta.

Wala sijawahi kuona mnyama simba akiitwa Diamond, Mr Blue au Afande Sele, ila hao wasanii wetu tayari wameshaingia kwenye malumbano ya kugombania haki ya kumiliki jina la mnyama huku majina yao ya kisanii yaliyowapa umaarufu hawatosheki nayo.

Mimi binafsi nimehudhunishwa sana na malumbano hayo, watu wanataka kazi, siyo malumbano, najua wengi wataumia ila lengo langu ni kujenga n si kubomoa, nimeenda mbali sana mpaka kukumbushia ya utotoni.

Tulikuwa tunagombania magari ya kupita barabarani ama ndege ikipita angani mpaka saa nyingine tunagombana mpaka kuzichapa kavu kavu.

Kiufupi wasanii hao waache utoto kugombania kitu ambacho akina uhalisia, watambue simba ni simba na mamba ni mamba, yaap Mkola Man Mwanatanga naondoka zangu na tukutane tena Wiki ijayo ila Happy Birthday Prince Hoza

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa