KIIZA, LYANGA WAIPELEKA SIMBA JIRANI NA UBINGWA

Na Salum Fikiri Jr, Tanga

Washambuliaji Hamisi Kiiza "Diego" na Danny Lyanga jioni ya leo wameiwezesha Simba Sc kuchanja mbuga na kukaribia kabisa ubingwa wa bara baada ya kuifungia mabao muhimu Simba ikiichapa Coastal Union mabao 2-0 uwanja wa Mkwakwani Tanga.

Simba ikishangiliwa na mashabiki wake ilijipatia mabao hayo moja kila kipindi na ikijiweka katika mazingira mazuri ya kunyakua kikombe cha ligi kuu bara.

Ushindi wa leo dhidi ya Wagosi wa kaya unawafanya Simba kufikisha pointi 57 huku ikiwa imecheza mechi 24, mshambuliaji Hamisi Kiiza anakuwa amefikisha magoli 19 ni sawa kama ameifikia rekodi ya mshambuliaji wa zamani wa timu hiyo ambaye kwa sasa yupo Yanga Amissi Tambwe aliyewahi kuwa mfungaji bora kwa kufunga magoli 19

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI