MWADUI FC YA JULIO YADAI ITAKUWA TIMU YA KWANZA KUIFUNGA YANGA KESHO

Kocha Mkuu wa Mwadui FC, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amesema wao ndiyo watakuwa wa kwanza kuitandika Yanga.

Mwadui FC ya mkoani Shinyanga inaikaribisha Yanga mjini humo keshokutwa Jumatano katika mechi ya Ligi Kuu Bara.

Julio amesema Mwadui FC itakuwa ya kwanza kuifunga Yanga ambayo imecheza mechi mfululizo bila ya kufungwa.

“Timu yetu ilianza kwa kuonekana haifai, ilidharauliwa na wengi walisema ni timu ya wageni.


“Lakini sisi ni watu tunaojua cha kufanya na utaona Yanga watakachokutana nacho,” alisema Julio.
“Tunajiamini, hata kama tunaheshimu uwezo wa Yanga lakini tuna kikosi bora kabisa,” alisema Julio.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI