Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Adebayor asema yuko tayari kuchezea Togo

Emmanuel Adebayor

Emmanuel Adebayor amemaliza kimya chake na kudai kuwa yuko tayari kuchezea Togo mechi ya kufuzu kwa Afcon dhidi ya Liberia Jumapili.

Nahodha huyo wa timu ya taifa ya Togo pamoja na wenzake wawili walikuwa wamekataa kujiunga na timu ya taifa iliyoitwa na kocha mpya Tom Saintfiet kwa maandalizi ya mechi yao ya kwanza ya kufuzu kwa Kombe la Taifa Bingwa Afrika bila kutoa sababu zozote.
 
Na straika huyo aliyepewa likizo na klabu yake ya Uingereza Tottenham ili akatatue matatizo ya kifamilia na kiakili kabla ya msimu kumalizika, amedokeza kuwa bado anajiandaa baada ya kutazama mechi ya kirafiki ambayo Togo walilazwa 0-1 na Ghana uwanja wa Accra Sports Stadium Jumatatu.

“Bila shaka nimekuwa nikijiandaa kuwa sawa kucheza soka tena kwa sababu umekuwa muda mrefu sana tangu nicheze dakika 90 za soka,” fowadi huyo lalisema alipoulizwa ni kwa nini hakuwa mmoja wa wachezaji waliokuwa uwanjani.


“Kuwa hapa hata kutazama mechi ni maridadi zaidi kwangu. Ninataka tu kurudi nyumbani na kuandaa mwili wangi kwa mechi ya wikendi [dhidi ya Liberia],” Adebayor akaongeza.

Kwake kuruhusiwa na kocha wao mpya kutoka Ubelgiji kujiunga na kambi sasa huenda likawa suala jingine kwani mdosi huyo wa zamani wa Malawi alikuwa amesema kwenye kikao na wanahabari baada ya mechi kwamba alilazimika kuchukua wachezaji waliojitokeza kuchezea taifa.

“Siwezi kumfuta au kumtaja mtu kwenye kikosi changu ilhali hata sijamuona kambini; hajafanya mazoezi na hajasema lolote kuhusu kushindwa kwake kujiunga na wenzake kambini,” akasema Saintfiet.
Togo watakaribisha nyumbani Liberia mjini Lome Jumapili alasiri.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa