Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Nooij: Stars fiti kuivaa Swaziland leo.

Timu ya Soka ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), leo inatarajiwa kushuka katika Uwanja wa Olympia Park, Rustenburg Afrika Kusini kuvaana na Swaziland katika michuano ya Baraza la Vyama vya Soka Kusini mwa Afrika (Cosafa).

Tanzania itashuka uwanjani katika mechi hiyo ya Kundi B, itakayopigwa majira ya saa 2:00 usiku kwa saa za Afrika Mashariki ikiwa kama nchi alikwa kwenye michuano hiyo.

Kocha Mkuu wa timu ya Taifa Stars, Mart Nooij, amesema kuwa wachezaji wake wako tayari kwa mchezo huo baada ya kufanya mazoezi kwa siku zote walizokuwa huko licha ya hali ya hewa ya kuwa ya baridi kali.


Nooij alisema wachezaji wake walitarajiwa kufanya mazoezi ya mwisho jana jioni kwa lengo la kujiandaa kuikabili Swaziland na kwamba wote wapo fiti.

"Hakuna mchezaji ambaye ameshindwa kufanya mazoezi licha ya hali ya hewa ya baridi, kila mmoja anajituma, ni dalili njema ndani ya timu kwa sababu tunahitaji kupata matokeo mazuri," alisema Kocha huyo.

Taifa Stars ambayo ni timu alikwa kwenye michuano hiyo inayofanyika kila mwaka itashuka tena Jumatano Mei 20 mwaka huu kuivaa Madagascar na itamaliza mechi zake za hatua ya makundi Ijumaa kwa kucheza na Lesotho.

Mshindi wa kila kundi ataungana na wenyeji Afrika Kusini, Msumbiji, Zambia, Ghana, Botswana na Malawi kucheza hatua ya robo fainali.

Kutakuwa na nusu fainali za aina mbili, kwanza za timu zilizofungwa katika robo fainali na zilizoshinda kwenye hatua hiyo.

Pia timu vibonde zitaendelea kupepetana hadi fainali yao ambayo itapigwa Mei 29, wakati fainali ya wakali itakuwa Mei 30.

Baada ya kumaliza mashindano hayo, Taifa Stars itaendelea na mazoezi kwa ajili ya mechi zake mbili zinazofuata dhidi ya Misri (mechi za mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika- Afcon) na baadaye Uganda kwenye michuano ya kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN).

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa