Ruka hadi kwenye maudhui makuu

CHAMA CHA WAZIRI MKUU ISRAEL CHASHINDA TENA UCHAGUZI

Benjamin Netanyahu waziri mkuu wa Israel wa chama cha Likud kilichoshinda uchaguzi mkuu wa tarehe 17 Machi 2015

Chama cha Likud cha Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu kimepata ushindi wa kushangaza katika uchaguzi mkuu wa Israel. Vimeripoti vyombo vya habari vya Israel.

Matokeo ya awali yalionyesha chama cha mrengo wa kushoto cha Zionist Union kupata mshitiko.


Huku kura nyingi zikiwa zimehesabiwa, Likud kinaonekana kupata viti 29 katika bunge lenye viti 120, huku chama cha Zionist Union kikiwa na viti 24.

Matokeo haya yakithibitishwa, itaonyesha kuwepo kwa serikali nyingine ya mseto itakayoongozwa na Bwana Netanyahu.
Yitzhak Herzog kiongozi wa chama cha mrengo wa kushoto cha Zionist Union

Bwana Netanyahu atahitaji kuungwa mkono kutoka vyama vingine ili kuunda serikali ya mseto.

Katika hotuba kwa wafuasi wake mjini Tel Aviv baada ya kufungwa kwa vituo vya kupigia kura Jumanne, Bwana Netanyahu amesema tayari amezungumza na viongozi wa vyama vingine vyenye mrengo wa kulia kuhusu kuunda serikali mpya "bila kuchelewa".

Bwana Netanyahu amehodhi siasa za Israel kwa muda mrefu katika kipindi cha miaka 20.

Kiongozi wa muungano wa vyama vya mrengo wa kushoto wa Zionist Union Yitzhak Herzog amekishutumu chama tawala cha Likud kwa kudidimiza viwango vya maisha ya raia wa Israel na amekuwa akipiga kampeni dhidi ya sera za nje za Bwana Netanyahu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa