Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KASEJA AWAAMBIA YANGA MSINITANIE MIMI BADO JANGWANI.

Mlinda mlango Juma Kaseja ameshtushwa na habari za kutimuliwa kwake na Yanga na kudai yeye hatambui maamuzi hayo kwani yametolewa nje ya muda muafaka wa usajili pili hajapewa barua ya kufukuzwa kwake.

Kaseja amesema yeye bado mchezaji halali wa Yanga na hatambui suala la kutimuliwa kwake.

Juzi uongozi wa Yanga ulitangaza kuachana na mlinda mlango Juma Kaseja kwa madai hajaripoti kwenye kituo chake cha kazi kwa muda mrefu na hajulikani halipo.


Kupitia kwa mkuu wa idara ya habari na mawasiliano wa Yanga Jerry Muro amesema Yanga imeamua kuachana na Kaseja kwakuwa alikuwa mzigo kwao.

Kaseja aliingia matatizoni na klabu yake akiidai fedha zake za usajili zilizosalia ambazo ni mil 20, lakini uongozi wa Yanga ulimalizana naye kwa kumwekea ktk akaunti yake fedha hizo.

Kaseja aliendelea kulumbana na Yanga safari hiyo akilalamikia kitendo cha kuwekwa benchi na kudai wamekiuka mkataba waliokubaliana ambao ulikuwa unasema atakuwa kipa wa kwanza.

Lakini uongozi wa Yanga umekiuka masharti ya mkataba na kumwambia mwenye suala ya kuamua nani awe kipa wa kwanza ni mwalimu kitendo kilichopelekea yeye kusugua benchi karibu mechi zote ilizocheza Yanga zikiwemo za kirafiki.

Juzi uongozi wa Yanga ulitangaza kuachana naye na kuna mipango ya kutaka kumfungulia kesi ya kudai fidia kwa madai kuwa Kaseja amevunja mkataba kwa kutoweka kwenye eneo lake la kazi jambo ambalo Kaseja anapinga na kusema yeye anatambua ni mchezaji halali wa Yanga na walka hajapewa barua ya kuachwa na akipewa atazungumza na waandishi wa habari

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa