Ruka hadi kwenye maudhui makuu

YANGA HAWATOKI JUMAMOSI- MTIBWA SUGAR

Uongozi wa Mtibwa Sugar umesema hautishwi na kipigo cha 3-0 ambacho Yanga imekitoa kwa Azam FC 3-0 kabla ya mechi yao ya kwanza ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu huu itakayozikutanisha kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro Jumamosi.

Ikitoka kushiriki michuano ya Kombe la Kagame, Azam FC ilikubali kichapo hicho dhidi ya kikosi cha Yanga kinachonolewa na kocha wa zamani wa timu ya Taifa (Taifa Stars) katika mechi ya Ngao ya Jamii iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Jumapili.


Kocha Mkuu wa Mtibwa Sugar, Mecky Mexime, jana alizungumza kwa njia ya simu kutoka Manungu, Morogoro kuwa kikosi chake kimejiandaa vema na mchezo huo na anaamini ataendeleza rekodi yake nzuri kila anapokutana na Yanga kutokana na kuzijua mbinu za kocha wao.

Maxime alisema hana wachezaji wenye majina 'makubwa' lakini wana uwezo wa kuikabili Yanga na timu nyingine kwenye ligi hiyo ambayo inatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kuanzia mechi ya kwanza hadi ya mwisho wa msimu.

Alisema Yanga inatakiwa kujipanga na kujiandaa kwa sababu mechi hiyo haitakuwa na 'mteremko'.

Aliwataka waamuzi watakaopewa nafasi kuchezesha mechi hiyo kuwa waadilifu kwa kufuata sheria 17 za mchezo huo ili mshindi atakayepatikana awe ni wa haki bila ya malalamiko ya upande wowote.

"Tunaendelea na maandalizi kama programu yetu tulivyoiandaa, kwetu mechi hiyo ni ya kawaida, hatuiwazii kama ambavyo wao wanatufikiria, huyo Jaja (Genilson) akifika Morogoro atakuwa 'Jojo', alisema Mexime.

Aliongeza kuwa anafahamu mbinu za Kocha Mkuu wa Yanga, Mbrazil, Marcio Maximo, hivyo kwake amekuwa na kazi nyepesi kuwaandaa wachezaji wake jinsi ya kuwakaba nyota wa Yanga.

"Najivunia wachezaji wangu, wengine wapya tumesajili kutoka Ligi Daraja la Kwanza lakini wanauwezo na wataonyesha kuwa Tanzania ina vipaji na klabu zisikimbilie kusajili wageni," aliongeza nahodha huyo wa zamani wa timu ya Taifa (Taifa Stars) ambaye pia aliwahi kuwa chini ya Maximo.

Mbrazil huyo amejerea nchini na kupewa mkataba wa miaka miwili akirithi mikoba ya Mholanzi Hans van Pluijm, ambaye aliondoka Yanga baada ya kupata kazi Saudi Arabia.

Kwa miaka mitano sasa Yanga haijawahi kushinda dhidi ya Mtibwa kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro huku timu hiyo inayonolewa na nahodha wake wa zamani na Taifa Stars, Mexime ikiwa ni moja ya timu zilizoipoteza maboya Yanga katika harakati zake za kutetea taji la VPL msimu uliopita iliyoupoteza kwa Azam FC.

Mara tu baada ya mechi yao dhidi ya Azam, Maximo alisema kikosi chake ambacho jana kilirejea tena kambini baada ya kupata mapumziko ya siku moja, kitakuwa na wakati mgumu dhidi ya Mtibwa Jumamosi.

"Nimeelezwa kwamba Yanga haijawahi kuifunga Mtibwa kwa muda mrefu nje ya Dar es Salaam. Jumamosi itakuwa mechi nzuri na ngumu kwa sababu Mecky (Mexime) anazifahamu mbinu zangu kwa kiasi kikubwa maana alikuwa nahodha wangu Taifa Stars," alisema Maximo.

Mtibwa ambao hawajawahi kutwaa ubingwa wa VPL tangu wautwae kwa mara ya mwisho mara mbili mfululizo 1999 na katika mwaka wa mabadiliko ya karne, wamekuwa wakionesha upinzani mkali kwenye Uwanja wa Jamhuri wanapocheza dhidi ya timu kongwe na zenye mashabiki lukuki nchini, Simba na Yanga.

Timu hiyo inayomilikiwa na kiwanda cha sukari cha Mtibwa Sugar chenye maskani yake Manungu, Turiani nje kidogo mwa mji wa Morogoro, imekuwa ikisifika kwa kuibua vijana wengi wenye vipaji ambao hata hivyo huwa haidumu nao kwa kipindi kirefu kabla hawajachukuliwa na Simba na Yanga.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa