Ruka hadi kwenye maudhui makuu

PHIRI AMPONDA LOGARUSIC, LAKINI WABANWA MBAVU NA NDANDA

Kocha mkuu wa Simba ambaye yupo katika mwezi wa kwanza wa mkataba wa mwaka mmoja, Patrick Phiri amesema aliikuta timu hiyo ikiwa na mapungufu mengi.

Phiri alichukua majukumu ya kuifundisha Simba baada ya uongozi wa rais Evans Aveva kumtimua Zdravko Logarusic 'Loga' kutokana na kukosa mafanikio ndani ya timu hiyo.

Mbali na kutofanya vizuri, kocha huyo pia alikuwa akilalamikiwa na wachezaji na baadhi ya viongozi kwa kutukana wachezaji na kuwafokea kupita kiasi.

Akizungumza mwishoni mwa wiki, Phiri alisema kikosi cha timu hiyo kilikuwa na mapungufu mengi, ikiwamo kukosa uimara katika ulinzi na kiungo.


"Wakati tupo Zanzibar nilifanyia kazi mapungufu niliyoyaona... timu haikuwa nzuri na hakukuwa na muunganiko mzuri," alisema.

"Lakini kwa sasa timu imekamilika kwa kiasi kikubwa na mpira unachezwa," alisema Phiri.

Alisema kuwa kila idara imekamilika kwenye kikosi chake isipokuwa mapungufu madogo madogo kwenye safu ya ushambuliaji.

"Tunatengeneza nafasi nyingi lakini umaliziaji umekuwa si mzuri, bado sijaridhishwa.
"Ni mambo madogo na nitaanza kuyafanyia kazi tukitoka Mtwara."

Simba ilikuwa Mtwara ambako jana ilicheza mechi ya kirafiki na Ndanda iliyopanda daraja la ligi kuu msimu huu kwa mara ya kwanza katika historia yake.

Wakati huo huo Simba jana ilishindwa kutamba mbele ya timu iliyopanda daraja la Ndanda FC ya Mtwara baada ya kutoka sare ya 0-0 kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona katika mchezo wa kirafiki wa kuadhimisha siku ya Ndanda Day

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa