Ruka hadi kwenye maudhui makuu

PHIRI AIPELEKA SIMBA RWANDA

Wakati kocha wa Simba, Patrick Phiri, akisema kikosi cha timu yake sasa ni sawa na 'moto usioshikika', timu hiyo inasaka wapinzani kutoka Rwanda baada ya kufutika kwa mechi yao iliyopaswa kuchezwa keshokutwa Jumatano dhidi ya Big Bullets kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza jana, Phiri, alisema kuwa kikosi chake kimeiva na kiko tayari kuanza msimu mpya wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara ambayo itaanza Septemba 20 mwaka huu.

Phiri alisema kuwa kiwango kilichoonyeshwa na timu yake katika mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya Gor Mahia ya Kenya kilimfurahisha na kilikuwa cha juu.


Mzambia huyo mwenye rekodi ya kuipa Simba ubingwa wa Bara bila kufungwa katika msimu wa mwaka 2008/2009 alisema anaamini Simba itarejesha heshima waliyoipoteza miaka miwili iliyopita.

Alisema kwamba kila mchezaji anajituma kuonyesha kiwango chake ili kuisaidia timu na kuongeza kuwa ushindani wa namba ni mkubwa katika kikosi chake.

"Nina furaha na kiwango cha timu yangu, hii inaonyesha vijana wako tayari kwa ligi na hawana wasiwasi...Simba ni moto sasa," alisema Phiri.
Kocha huyo aliongeza kuwa baada ya jana kuwapa mapumziko wachezaji wake, leo timu hiyo itaingia kambini Kunduchi kuendelea na mazoezi.

Naye Rais wa Simba, Evans Aveva, alisema jana kuwa uongozi umefurahishwa na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Gor Mahia na kiwango cha timu kilivyoonyeshwa.

Aveva alisema kuwa baada ya mechi  kuahirishwa kwa keshokutwa iliyokuwa dhidi ya Big Bullets, kikosi cha Simba kitasafiri kuelekea Mtwara kucheza mechi nyingine dhidi ya Ndanda FC katika kuadhimisha siku ya Ndanda Day.

Alisema timu itaondoka jijini Dar es Salaam Ijumaa na itakuwa ni nafasi nyingine ya kuwapima wachezaji ambao hawajapata nafasi ya kuonekana katika mechi zilizotangulia.

Aliwashukuru na kuwaomba mashabiki na wanachama wa Simba kuendelea kujitokeza kuiangalia timu yao katika mechi za kirafiki wanazocheza ndani na nje ya Dar es Salaam.

Simba ilizifunga 2-1 Kilimani City, 2-0 Mafunzo na 5-0 KMKM, mechi zote zikipigwa Uwanja wa Amaan, Zanzibar kabla ya juzi kuifumua 3-0 Gor Mahia.

Simba itaanza kampeni ya kuwania ubingwa wa Ligi Kuu ya Bara msimu ujao kwa kuikaribisha Coastal Union Septemba 21 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa