Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MESSI AANDIKISHA REKODI NYINGINE BARCELONA



Nyota maarufu wa Argentina, Lionel Messi, alifunga bao lake la 400 katika mchezo wa kulipwa huku mwenzake wa Brazil, Neymar, akitia kizimbani matatu kwenye ngoma ambayo magwiji wa Uhispania, Barcelona, waliadhibu vikali Granada 6-0 Jumamosi.
Mabingwa Atletico Madrid walipanda hadi nafasi ya pili, alama mbili nyuma ya Barca baada ya kupatia Sevilla kichapo chao cha kwanza kwa kuwafunga magoli manne bila jibu.

Naye mchezaji bora zaidi duniani, Cristiano Ronaldo, aliendelea kuwa hatari mbele ya lango baada ya kufungia Real Madrid kwenye ushindi wao wa 2-0 ugenini Villareal kubakia alama nne nyuma ya viongozi na maadui wao wakuu.

Barca waliendeleza mwanzo wao bila kufungwa huku wakionesha makali yao katika mashambulizi yalioongozwa na Messi na Neymar.


Neymar alifungua udhia dakika ya 26 baada ya kutimuka mbele na kuachilia mkwaju uliobadilishwa mwelekeo na kuishia kizimbani na beki Jean-Sylvain Babin.

Messi aliunganisha goli la saba musimu baada ya krosi yake kupata kichwa cha Ivan Rakitic aliyefunika mpira wavuni kabla ya Neymar kutia ndani la tatu kufikia kipindi cha kwanza.

Barca waliendelea na mshambulizi mazito na Neymar alipata lake la tatu baada ya kupokea mpira kutoka kisigino cha Messi kabla ya staa huyo wa Argentina kukamilisha adhabu alipopokonya ngome ya Granada mpira na kutimuka hadi kisanduku na kuzamisha ndani ya neti.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa